mwambelablog

Wednesday, 30 November 2022

RC CHALAMILA AWAONYA WAJUMBE WA BARAZA LA ARDHI NA NYUMBA

 

Pichani:Mkuu wa mkoa wa Kagera Albert John Chalamaila akimuapisha mjumbe wa baraza la ardhi na nyumba wilaya ya Kyerwa.

Na Lydia Lugakila, 

Kagera.


Mkuu wa mkoa wa Kagera Albert John Chalamaila amewaapisha wajumbe wa wanne wa baraza la ardhi na nyumba wilaya ya Kyerwa huku akiwaoya kukataa maelekezo ambayo yapo nje ya misingi ya kisheria yanayoweza kusababisha kukosekana kwa haki za watanzania.


Akizungumza baada ya kuwaapisha wajumbe hao ambao waliteuliwa hivi karibuni na waziri mwenye dhamana amesema wanatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na sheria bila kuingiliwa na chombo chochote ili wawe wazalendo katika nchi yao.


"Fanyeni kazi zenu kwa weledi mkishakuwa na maelekezo kwa hiki kifanyike hivi mara kile vile ninyi rudini katika misingi ya sheria ili kujua kama kitu hicho kipo kisheria , fanyeni kwa mujibu wa taratibu epukeni kuelekezwa elekeza na kila mtu mtaharibu kazi yenu, na kuwakosesha haki watanzania" alisema.


Chalamila amesisitiza pia wajumbe hao kujiepusha na rushwa badala yake watoe haki na kupunguza mashauri ambayo yamerundikana katika mabaraza mengi bila sababu za msingi.


" Kumekuwa na mlolongo mkubwa wa kesi zinazohusiana na masuala ya ardhi na mirathi toeni elimu kuhusiana na mambo yatakayoweza kupunguza mashauri, tumieni Muhimili wa vyombo vya dini katika kupunguza masuala mengi yaliyo rundikana kwenye mabaraza" alisema 


Aidha Mwenyekiti wa baraza la ardhi wilaya ya Kyerwa Denis David amesema kuwa kuwepo kwa baraza hilo kumesaidia wananchi wengi kwani swali walikuwa wakifuata huduma hiyo wilaya jirani ya Karagwe.


Naye Mkuu wa wilaya ya Kyerwa Rashid Muhamed Mwaimu amempongeza Rais Samia kwa kuwasogezea huduma hiyo ya kimahakama wilayani hapo kwani wananchi wake walilazimika kutembea umbali mrefu wa kilometa mia moja kwenda Karagwe ambapo pia alisisitiza watimize majukumu yao kizalendo 


Wajumbe walioapishwa ni Ester Mutafuta Ezra Lugakila Joyleth Godwin na Elias ambapo wameahidi kutenda haki huku kipaumbele cha kwanza likiwa ni kumpinga adui Rushwa .

OFISI YA WAZIRI MKUU KITENGO CHA MAAFA YATIMIZA AHADI KAGERA,

 



Na Lydia Lugakila,

 Kagera


Ofisi ya waziri mkuu kupitia kitengo cha maafa imeanza kutoa mafunzo ya uokoaji kwa wavuvi kutoka wilaya ya Bukoba Misenyi ikiwa ni hatua ya kuwaongezea uwezo wa kufanya uokoaji wakati yanapotokea majanga.


Akifungua mafunzo hayo mkuu wa mkoa wa Kagera Albert Chalamila amesema kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la waziri mkuu alilolitoa baada ya kutokea ajali ya ndege precision Air  iliyotokea Novemba 6  mwaka huu ndani ya ziwa Victoria na kusababisha vifo vya watun19 na 24 kunusurika.


Amesema kuwa  anaishukuru ofisi ya Waziri  Mkuu kitengo Cha maafa kuanza  kutoa Mafunzo hayo yatakayosaidia kuongeza ujuzi na uhodari katika uokozi kwa vikundi vya  wavuvi mkoani hapa huku akitoa wito kwa jamii ya Watanzania kuacha tabia ya kubeza juu ya juhudi zilizofanyika katika kipindi Cha ajali hiyo.


Naye mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Maafa kutoka Ofisi ya waziri mkuu, Luten Kanali Selestine Masalamado amesema kuwa  wavuvi kutoka mkoani Kagera  walioshiriki kufanya uokoaji wanashiriki mafunzo hayo maalumu kwa kipindi cha  siku 7 ili waweze kuwapa mafunzo na uzoefu kutoka kwa wataalam ili kujua namna nzuri ya kuweza kumuokoa mtu anayepata ajali kwenye maji pamoja na utayari wa kukabiliana na majanga katika ziwa yanapotokea.



Ameongeza kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kupunguza athari zinazojitokeza ziwani, ikiwa ni pamoja na kuokoa maisha ya watu na kupunguza upotevu wa mali wakati wa ajali.


Aidha kwa upande wao wavuvi hao akiwemo Hashim Rashid na Taufic Shariff wameishukuru serikali kwa mafunzo hayo kwani yatawanufaisha mbali na kuokoa wameongeza ufanisi wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao.


Wavuvi hao wamepata vifaa vya uokoaji vitakavyowasaidia kufanya kazi ya uokoaji kwa urahisi pamoja na kujifunza namna ya kuvitumia kuokoa watu ajali inapotokea ambapo

TET YAFANYA ZIARA YA MAFUNZO NCHINI RWANDA

 


Kutoka Rwanda

Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) pamoja na wajumbe wa kamati ya Kitaifa ya wataalamu inayosimamia uboreshaji wa Mitaala ya Elimumsingi, Sekondari ya Juu na Ualimu leo tarehe 29/11/2022 imetembelea Bodi ya Elimu ya Nchini Rwanda (Rwanda Basic Education Board) kwa lengo la kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo uandaaji wa  Mitaala yenye kujenga ujuzi.


TET ipo katika ziara nchini Rwanda kuanzia tarehe 28/11/2022 hadi 2/12/2022  kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu maboresho ya Mitaala yanayoendelea nchini.


Katika ziara hiyo Bi Joan Murungi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Elimu Rwanda (REB) aliwasilisha kazi mbalimbali zinazofanywa na Bodi hiyo na namna Rwanda inavyotekeleza mitaala inayojenga umahiri  ( Competence Curriculum Based)


Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Kitaifa ya Mitaala Prof.Makenya Maboko amesema kuwa,Serikali ya Tanzania kupitia TET kwa sasa ipo inafanya maboresho ya mitaala itakayosaidia kuondoa tatizo la ukosefu wa ajira  kwa kumuandaa mhitimu mwenye ujuzi wa kujiajiri na kumudu maisha ya siku kwa siku.


"Tumekuja kujifunza nchini namna Rwanda inavyoandaa na kutekeleza Mitaala yenye kumjengea mwanafunzi ujuzi. Hili ndilo lengo la kufanya mapitio haya makubwa ya mitaala na kiu ya wadau wengi ni kuwa na mitaala itakayowawezesha wahitimu kuwa na ujuzi". Amesema Prof.Maboko.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TET Dkt.Aneth Komba amesema, uzoefu utakaopatikana utasaidia katika mapitio ya mitaala yanayoendelea.


"Kwa sasa tayari TET tumeandika rasimu ya mtaala na mihutasari lakini tumekuja hapa kupata uzoefu juu ya uandaaji na utekelezaji wa mitaala yenye kumjengea mhitimu uwezo wa kujiajiri na kumudu maisha ya kila siku" Amesema Dkt.Aneth.


Nchi ya Rwanda imefanya maboresho ya mtaala mwaka 2015 na kuweza kuwa na Mitaala inayozingatia ujenzi wa umahiri.

WAGANGA WAKUU WAELEKEZWA KUBORESHA USIMAMIZI WA UTENDAJI HUDUMA.

 

Pichani:NAIBU WAZIRI wa Afya Dkt. Godwin Mollel akiongea na Waganga Wakuu wa Mikoa kuboresha usismamizi wa utoaji wa huduma za afya Nchini.

Na WAF - LINDI


NAIBU WAZIRI wa Afya Dkt. Godwin Mollel amewaelekeza Waganga Wakuu wa Mikoa kuboresha usismamizi wa utoaji wa huduma za afya katika vituo vya kutolea huduma wanavyosimamia nchini.


Dkt. Mollel ametoa rai hiyo leo Novemba 30, 2022 wakati akifunga Mkutano wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Waratibu wa Mikoa wanaosimamia Masuala ya Ukimwi nchini uliofanyika siku moja kabla kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani.


"Tanzania imepiga hatua kubwa kuboresha huduma za afya, lakini juhudi za ziada zinahitajika kuboresha zaidi ubora wa huduma tunazotoa, hivyo natoa rai kwenu kwenda kusimamia hilo ” amesema Dkt. Mollel.


Sambamba na hilo Dkt. Mollel amesema kuwa, wakati huu ambapo Serikali inalenga kwenda kwenye Bima ya Afya kwa wote ni vyema kwa watendaji katika vituo vya kutolea huduma za afya vya umma kuboresha zaidi huduma wanazotoa.


Kuhusu mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Virusi Vya Ukimwi, Dkt. Mollel amewapongeza watendaji pamoja na wadau wa Sekta ya Afya kusimamia vyema utekelezaji wa  afua za mapambano dhidi ya Ukimwi na kuiewezesha Tanzania kupunguza kiwango cha maambukizi ya VVU kwa asilimia 62 toka mwaka 2010.


Aidha, Dkt. Mollel amewataka viongozi na watumishi kwa pamoja kuwajibika ipasavyo katika utoaji wa huduma bora ili kuweza kuokoa maisha ya Watanzania na kuwa na wananchi wenye afya njema wanaowajibika katika ujenzi wa nchi.


Sambamba na hilo ameendelea kusisitiza juu ya usimamizi mzuri wa dawa na kuhakikisha upungufu wa dawa haujitokezi katika vituo vyote vya kutolea huduma ili wananchi wasipate changamoto yoyote pindi wanapoenda kutafuta mahitaji. 


WAZIRI MKENDA APANIA MAGEUZI YA ELIMU

 

Pichani:Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda wakati wa kikao cha pamoja cha Menejimenti ya Wizara na ile ya VETA jijini Dodoma.

Kutoka,DODOMA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema mageuzi ya elimu yanayokuja yanakwenda sambamba na kuandaa mazingira ya kuhakikisha elimu ujuzi inapatikana.


Mkenda ameyasema hayo jijini Dodoma wakati wa kikao cha pamoja cha  Menejimenti ya Wizara na ile ya VETA chenye lengo la kujadili kwa pamoja rasimu ya  mkakati wa utekelezaji wa ujenzi wa VETA 63 za wilaya na moja ya mkoa.


Amesema moja ya eneo linaloangaliwa katika kutoa elimu ujuzi ni kupitia vyuo vya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) hivyo ni   vizuri kuwa na mikakati thabiti ya kuhakikisha VETA 63 za Wilaya na moja ya mkoa ujenzi unaanza.


 "Nataka twende pamoja, katika kuweka historia hii; tunakwenda kufanya mageuzi makubwa ya elimu kwa kuhakikisha  tunatoa elimu ujuzi, sasa kazi ya mapitio ya Sera  na Mitaala inakwenda vizuri na tuko tayari kufanya wasilisho kwa ajili ya mjadala wa Kitaifa, sasa nataka huku kwenye ujenzi wa VETA 63 ambako elimu ujuzi inapatikana kuende kwa kasi na kwa  wakati ,"amesema Prof. Mkenda


Amesema katika mwaka wa fedha 2022/23 Wizara imetenga fedha Bilioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa VETA hizo hivyo  kutaka   mkakati wa kuhakikisha ujenzi unaanza mapema na kujengwa kwa usahihi kwa kuzingatia taratibu zote husika.


Akizungumzia ujenzi wa Kampasi za Vyuo Vikuu katika mikoa 14 kupitia Mradi wa HEET Mhe. Mkenda amewataka Wakandarasi waliopo wizarani kuhakikisha wanafanya ufuatiliaji na kushirikiana na  na Vyuo Vikuu kujua mikakati iliyowekwa na Vyuo mama kuhusu ujenzi huo ili kazi iweze kwenda kwa haraka.


Akizungumzia maandalizi ya ujenzi wa VETA hizo Mhandisi George Sambali kutoka VETA  amesema mpaka sasa kati ya wilaya 63 zinazojengewa VETA wilaya 59 tayari zina maeneo.


CHANJO YA POLIO AWAMU YA NNE KUANZA KESHO TAREHE 1/12/2022.

 



Pichani: Afisa Program ya Chanjo Bi. Lotalis Gadau kutoka mpango wa Taifa wa Chanjo leo Novemba 30, 2022 wakati wa Semina elekezi kwa Wanahabari jijini Dodoma 


Na Deborah  Lemmubi - Dodoma.


Kampeni ya awamu ya nne ya Chanjo ya Polio kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano kuanza kesho ambapo watoto takribani 14,690,597 wanatarajiwa kupata chanjo hiyo.


Ambapo Kampeni hiyo inatarajiwa kuanza kesho December 1 hadi 4, 2022 na itafanyika nchi nzima , ikiwa Polio ni miongoni mwa magonjwa hatarishi zaidi kwa watoto ambapo virusi vya polio huvamia mfumo wa Neva na madhara yake husababisha kupooza au hata Kifo.


Hayo yamebainishwa na afisa Program ya Chanjo Bi. Lotalis Gadau kutoka mpango wa Taifa wa Chanjo leo Novemba 30, 2022 wakati wa Semina elekezi kwa Wanahabari jijini Dodoma inayohusu kutoa elimu kuelekea katika kampeni ya polio ambapo amesema kampeni hiyo itakuwa ni nyumba kwa nyumba.

Pichani:  Wanahabari leo Novemba 30, 2022 wakati wa Semina elekezi jijini Dodoma.


"Kwa utoaji wa chanjo za matone ya Polio ikilenga Watoto kuanzia Umri chini ya Miaka mitano sambamba na Timu za wachanjaji ambapo kutakuwepo na waangalizi wa kujitegemea katika Kila Mkoa nchini ili kukamilisha zoezi hilo"


Aidha Bi Lotalis ametaja njia za maambukizi ya ugonjwa huo sambamba na dalili ikiwa ni pamoja na homa, uchovu, maumivu, ya kichwa, kutapika, kukakamaa shingo na maumivu ya Viungo.


“Ugonjwa huu huambukizwa kwa kuingia mwilini kwa njia ya mdomo, kunywa Maji,au chakula ambacho kimechafuliwa na kinyesi kutoka kwa Mtu aliyeambukizwa virusi hivyo na virusi huongezeka ndani ya utumbo na hutolewa na mtu aliyeambukizwa kwenye kinyesi, ambacho kinaweza kupitisha virusi kwa wengine”


Pia ameeleza Hali ilivyo kwa sasa juu ya ugonjwa wa Polio katika maeneo mbalimbali ndani ya Bara la Afrika.


“ambapo amesema, Zambia tayari kuna kisa kimoja, wenyewe wanajiandaa na awamu ya Tatu,Msumbiji wa visa 8 na wanajiandaa na awamu ya 6 Malawi wana kisa 1 na wanajiadaa na awamu ya 5,na kwetu Tanzania tunamshukuru mungu bado hatujapata kisa, lakini bado hatujalemaa, bado tunaendelea na ufuatiliaji kwa kuchukua Sampuli kuhakikisha kwamba tunapeleka maabara mwisho wa siku watoto wetu wawe salama.DRC CONGO bado kuna vimlipuko vya hapa na pale lakini ambao tulienda nao sambamba tokea tunaanza mwanzo ni Malawi, Msumbiji, Zimababwe na Zambia”


Pia ameeleza mikakati inayotumika katika kuhakikisha wanatokomeza ugonjwa huo hapa nchini ikiwa ni pamoja na kufanya kampeni za kutoa elimu itakayoambatana na utoaji wa Chanjo.


“Tunachojitahidi ni kuonyesha kwamba tunaimarisha utoaji wa chanjo za kila siku kuhakikisha kwamba watoto wetu wanakamilisha Ratiba zao za chanjo ili endapo hata Kirusi kikija kikimkuta mtoto ameshapata kinga kamili kinakuwa hakina nafasi na kwa awamu hii tunalenga kuwafikia watoto wapatao Millioni 14 laki sita na Tisini, Mia tano Tisini na Saba kwa awamu hii ya nne”


Bi lotalis amehitimisha kwa kusema kuwa zoezi hili litafanyika kwa kupita nyumba kwa nyumba na kisha nyumba ambayo itakuwa imepata chanjo itawekwa alama ya Tiki ili kuonesha tayari imekwisha kupata huduma ili kurahisisha utekelezaji wa zoezi hilo na kuepusha usumbufu wa foleni na upotevu wa muda.

Monday, 28 November 2022

WACHIMBAJI WADOGO WASHAURIWA KUPATA TAARIFA ZA KIJIOLOJIA KTOKA MAENEO SAHIHI

 

Na Deborah  Lemmubi - Dodoma.


Wachimbaji wadogo wa Madini Nchini wameshauri kuwa na tabia ya kupata taarifa za Kijiolojia maeneo ambayo sahihi hasa Taasisi ya Jiolojia Tanzania ili kuepuka Uchimbaji wa kubashiri na uharibifu wa Mazingira.


Hayo yamesemwa na Kamishna Msaidizi Uendelezaji wa wachimbaji wadogo kutoka Wizara ya Madini Mhe Francis Mihayo akiwa katika Jukwaa la sekta ya Uziduaji lililoandaliwa na Shirika la HakiRasilimali lililofanyika Jijini Dodoma.



"Kwa ushauri Watanzania wapende kutafuta taarifa maeneo ambayo ni sahihi,kwa fursa hii napenda nitambulishe kuwa tuna Taasisi ya Jiolojia (GST) inawezekana hawaijui au hawajui majukumu yake, lakini kikubwa wao ndio wana jukumu la kufuatilia taarifa za kijiolojia"


"Na kuongeza kuwa, Tukisema taarifa za kijiolojia ni taarifa za Madini yote ambayo yanapatikana Tanzania kwani Taasisi hii wanatengeneza ramani za madini yote,wana taarifa zote na wanafanya Tafiti zote, Mfano ukitaka kujua Dhahabu inapatikana wapi wao watakwambia Dhahabu inapatikana mahali fulani iwe ni Kanda ya Ziwa au kwingineko"


Aidha Mhe Mihayo amewataka wachimbaji wadogo kuendelea kutunza Mazingira katika maeneo ya kazi zao.


"Suala la kutunza Mazingira ni muhimu kwa Wachimbaji hawa hasa pale anapotaka kuhama kutoka eneo moja kwenda jingine ni vema akahakikisha pale anapotoka Mazingira yapo sawa kwa kufukia mashimo yote ikiwezekana apande hata miti"


Kwa upande wa CPA Ludovick Uttoh ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uhamasishaji ya Uwazi na Uwajibikaji katika sekta ya Uziduaji (MSG) amesema Uwazi na Uwajibikaji wa kweli ni muhimu katika kukuza ongezeko la Uchumi wa Nchi kupitia sekta hii ya Uziduaji.


"Katika miaka mitatu/minne iliyopita uchangiaji wa hii sekta kwa uchumi wa Nchi ni asilimia 3.2, mwaka jana ilifika asilimia 7 na kwa lengo itakapofika 2025 matarajio na mipango ya Serikali kwamba hii sekta iweze kuchangia kwa asilimia 10, lakini hatutafika huko kama hakutakuwa na Uwazi na  Uwajibikaji wa kweli katika usimamizi wa hii sekta"


Naye Eng Theonista Mwasha ambaye ni Mwanamke wa kwanza katika Sekta hii ya Uziduaji na Katibu Mtendaji kutoka Taasisi ya kuendeleza Uchimbaji mdogo Tanzania amesema Wanawake wanachangamoto ya kutojiamni katika sekta hii ya uziduaji inayopelekea Wanawake kutofaidika kama inavyotakiwa.


"Wanawake wamekuwemo katika hiyo sekta kwa muda mrefu lakini wameshindwa kufaidika kama inavyotakiwa,kwasababu ya uelewa pia wamejiona wao wako nyuma kama sekta nyingine. Kimila na Desturi Mwanamke anajiona kwamba hiki mimi siwezi kwahiyo tunawajengea uwezo wa kujiamini ili kama wameamua kufanya kazi wafanye kwa nguvu zao zote na akili zao zote pia wajiamni"


Jukwaa hili la Uziduaji ambalo kuratibiwa na Shirika la HakiRasilimali hufanyika kila mwaka na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta hii ili kujadili mambo tofauti ikiwemo kuangazia changamoto wanazopata wachimbaji wadogo na kuona  namna ya kuzitatua.

RESHAPING INDUSTRIES WITH AI:HUAWEI CLOUD LAUNCHES PANGU MODELS 3.0 AND ASCEND AI CLOUD SERVICES

Zhang Ping'an, Executive Director of Huawei and CEO of Huawei Cloud, announcing Pangu Models 3.0. [Dongguan, China, July 7, 2023] The...